GOOD NEWS: Ibrahim Ajibu Apata Mtoto wa Kike, Atoa Kauli Nzito
Uongozi wa klabu ya Yanga umetangaza kuwa familia ya Mshambuliaji wake, Ibrahim Ajibu, imejaaliwa kupata mtoto wa kike.
Ajibu alishindwa kusafiri na kikosi cha Yanga kuelekea Algiers, Algeria kwa ajili ya mechi ya mkondo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya U.S.M Alger.
Mchezaji huyo amesema kuwa ujauzito wa mkewe umepitia changamoto mbalimbali, jambo lililopelekea hofu kubwa kwake lakini ameeleza kumshukuru Mungu kwa kufanikiwa kujifungua salama.
Mbali na mkewe kupata mtoto, Ajibu amesema kuwa ameumizwa na baadhi ya mashabiki waliomtumia ujumbe mfupi wa mane kupitia simu wakimuandama kuwa hajasafiri na timu.
GOOD NEWS: Ibrahim Ajibu Apata Mtoto wa Kike, Atoa Kauli Nzito
Reviewed by NARIAMI
on
May 05, 2018
Rating: 5
No comments: